Sehemu ya Ukraine iliyokaliwa yahimizwa kupiga kura katika uchaguzi wa Urusi
Urusi imezindua kampeni mbalimbali kuwarai wakazi wa maeneo yanayokaliwa kwa mabavu ya Ukraine kupiga kura katika uchaguzi wa rais wa Urusi.
Kwa mara ya kwanza, upigaji kura wa kitaifa unafanyika kwa muda wa siku tatu (15-17 Machi), lakini upigaji kura wa ziada wa mapema tayari umeanza katika sehemu zinazokaliwa na mikoa minne ya Ukreni: Zaporizhzhia, Kherson, Donetsk na Luhansk.
Mkazi mmoja alilalamikia washirika wanaoiunga mkono Urusi na masanduku ya kura wakipita nyumba hadi nyumba kutafuta wapiga kura walioandamana na wanajeshi waliojihami.
Vladimir Putin hakika atashinda muhula mwingine wa madaraka, lakini kujitokeza kwa wingi kutasaidia juhudi za Urusi kuhalalisha utawala wake unaoendelea.
Pia ingetumika kuhalalisha uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.
Vladimir Putin ni mmoja wa wagombea wanne kwenye kura, lakini hakuna hata mmoja wekati ya hao wengine anayeleta ushindani wa kweli.
Wakosoaji wake wote waliozungumza sana ama wamelazimishwa kwenda uhamishoni, kufungwa jela, au wamefariki.
Kulazimishwa kupiga kura.
Ijapokuwa mamlaka yenye kufanya uvamizi imeweka vituo vya kupigia kura, wapiga kura hawatakiwi kuvitembelea kwani mamlaka hizo hizo zimetuma watu wakiwa na masanduku ya kupigia kura majumbani mwao.
Waukraine walio chini ya uvamizi pia wanawekwa chini ya shinikizo kupitia kampeni ya wafuasi wa kura iitwayo InformUIK, iliyobuniwa kuwajulisha kuhusu utaratibu wa upigaji kura, pamoja na wagombea wote.
Inatafuta kutembelea wakaazi wote waliobaki wa mikoa inayokaliwa na Urusi nyumbani - na wawakilishi wake mara nyingi hufuatana na watu wenye silaha.
BBC

Post a Comment