Biden na Trump kukutana tena katika uchaguzi wa urais baada ya kuteuliwa na vyama vyao
Rais wa Marekani Joe Biden na mtangulizi wake Donald Trump wote wamepata wajumbe wa kutosha kuteuliwa na vyama vyao katika uchaguzi wa mwezi Novemba.
Majimbo na Wanademokrasia wanaoishi nje ya nchi walishiriki katika uchaguzi wa mchujo siku ya Jumanne.
Matokeo hayo yanamaanisha kuwa wapiga kura wa Marekani wanakabiliwa na marudio ya uchaguzi wa urais wa 2020 katika muda wa miezi minane.
Uteuzi huo utafanywa rasmi katika makongamano ya chama msimu huu wa joto.
Rais huyo mwenye umri wa miaka 81 alisema Jumanne jioni kwamba "ameheshimiwa" wapiga kura wameunga mkono ombi lake la kuchaguliwa tena "katika wakati ambapo tishio la Trump ni kubwa kuliko hapo awali".
Akitoa mfano wa mwelekeo chanya wa kiuchumi, alidai kuwa Marekani ilikuwa "katikati ya kurejea" lakini inakabiliwa na changamoto kwa mustakabali wake kama demokrasia, na vile vile kutoka kwa wale wanaotaka kupitisha vikwazo vya utoaji mimba na kupunguza programu za ustawi wa kijamii.
"Ninaamini kwamba watu wa Marekani watachagua kuendelea kwa uwepo wetu katika siku zijazo," Bw Biden alisema katika taarifa kutoka kwa kampeni yake.
Uongozi ulimweka Bw Biden kifua mbele na hakukabiliwa na wapinzani wakubwa katika uteuzi wa chama chake.
Licha ya wasiwasi wa mara kwa mara kutoka kwa wapiga kura kwamba umri wake unapunguza uwezo wake wa kutekeleza majukumu ya urais, chama chake kilimuunga mkono.
Wakati huo huo, Bw Trump, 77, anasalia kupendwa sana na wapiga kura wa chama cha Republican, ambacho kimemfanya ashinde katika kila mchujo dhidi ya wapinzani wanaofadhiliwa vyema.
BBC

Post a Comment