Museveni azindua benki ya kwanza kabisa ya Kiislamu nchini Uganda
Benki ya Salaam Limited itakuwa taasisi ya kwanza kutoa ufadhili wa Kiislamu nchini Uganda
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amezindua rasmi benki ya kwanza kabisa ya kibiashara ya Kiislamu nchini humo isiyo na riba.
Salaam Bank Limited, kampuni tanzu ya benki ya Djibouti, ni taasisi ya kwanza kutoa ufadhili wa Kiislamu nchini humo.
Bw Museveni alisema taasisi hiyo ina uwezo wa kuchangia pakubwa katika maendeleo ya sekta ya fedha Uganda na kuvutia wawekezaji zaidi Waislamu.
"Ninawahimiza kupigana na umaskini na kuunda utajiri," rais alisema muda mfupi baada ya kuzindua benki hiyo Jumatano katika mji mkuu, Kampala.
Mnamo Septemba mwaka jana, benki ya Salaam ilipewa leseni yake ya kwanza ya benki ya Kiislamu baada ya bunge la Uganda kupitisha sheria inayoidhinisha benki za Kiislamu, ambazo Bw Museveni alitia saini kuwa sheria.
Hairuhusiwi kulipa na kupokea riba katika benki ya Kiislamu, bali inategemea kugawana faida.

Post a Comment