Watanzania waishio nje ya nchi wanaleta nyumbani fedha kiduchu kuliko Wakenya

 


Watanzania wanaoishi nje ya nchi, maarufu kama Diaspora wanaingiza fedha kiduchu nchini, kuliko wenzao wa Kenya. Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa, wakati Watanzania hao wanaleta nyumbani kiasi cha shilingi bilioni 791, Kenya inaongoza miongoni mwa nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki, ambapo yenyewe hupokea kiasi cha shilingi Trilioni 10 kwa mwaka.

Somalia, ambayo muda mwingi iko vitani wenyewe kwa wenyewe, wananchi wake wanaleta nyumbani kiasi cha shilingi trilioni 4, huku Congo DR, ambayo na yenyewe muda mwingi iko vitani, inapokea shilingi trilioni 3.2.

Uganda yenyewe inapokea shilingi trilioni 3 kutoka kwa raia wake wa nje, wakati Sudan ya Kusini yenyewe wananchi wake walio nje huwaletea kiasi cha shilingi trilioni 2.7 na Rwanda, moja ya nchi zinazotajwa uchumi wake kupaa kwa kasi, hupokea kiasi cha trilioni 1.3.

 

No comments