Abiria na wafanyakazi 379 waokolewa ndege ikiteketea na moto Tokyo




Ni zaidi ya saa moja sasa tangu tulipoanza kupokea picha kutoka Uwanja wa Ndege wa Haneda mjini Tokyo ambapo ndege ya abiria ya Shirika la Ndege la Japan iliwaka moto ilipokuwa ikitua.

Haya ndio tunayojua kufikia sasa:

  • Watu wote 379 waliokuwa kwenye ndege - abiria na wafanyakazi - wameondolewa salama, kulingana na Shirika la Ndege la Japan.
  • Ndege hiyo nambari 516 inaaminika kuhusika katika mgongano na ndege ya walinzi wa pwani ya Japan ilipokuwa ikitua.
  • Vyombo vya habari vya Japan vinaripoti kuwa mtu mmoja aliyekuwa kwenye ndege ya walinzi wa pwani alitoroka, huku wengine watano wakiwa hawajulikani waliko.
  • Video na picha zilizochapishwa mitandaoni zinaonyesha ndege ya Japan Airlines ikiteketea kwenye barabara ya kurukia ndege, huku picha kutoka ndani ya ndege zikionyesha abiria wakiwa wamezingirwa na moshi mzito.
  • Ndege hiyo ilikuwa safarini kutoka Sapparo kwenye kisiwa cha Hokkaido, kaskazini mwa Japan, na ilitakiwa kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Haneda muda mfupi kabla ya 18:00 saa za ndani (09:00 GMT)
  • Mlinzi wa pwani anasema mazingira ya ndege hizo mbili kugongana "inachunguzwa"
  • Safari zote za ndege kutoka Uwanja wa Ndege wa Haneda zimesitishwa

No comments