Mradi wa kuzuia watu kuzama maji Ziwa Victoria watambulishwa Mwanza
Shirika la mazingira na maendeleo
EMEDO limeutambulisha mradi wa kuzuia watu kuzama maji katika Ziwa
Victoria kwa wadau mbalimbali wa uvuvi mkoani Mwanza.
Afisa
Mradi huo, Arthur Mgema amesema lengo ni kuzuia vifo vitokanavyo watu
kuzama maji katika Ziwa Victoria hasa wavuvi, watoto na wanawake
wachakataji wa mazao ya samaki/ dagaa ambao wako kwenye hatari zaidi.
Akifungua
kikao cha kuutambulisha mradi huo, Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Elikana
Balandya amesema matukio ya watu kuzama maji yanazuilika endapo kila
mmoja atatimiza wajibu wake.
Amesema kwa Mkoa Mwanza Serikali
inatekelezeka mpango wa BBT (Building Better Tomorrow) katika sekta ya
ufugaji na uvuvi hivyo mradi wa kuzuia kuzama maji katika Ziwa Victoria
utasaidia kutoa elimu ili kuzuia vifo zitokanavyo na kuzama maji.
Mradi
wa kuzuia kuzama maji katika Ziwa Victoria unatekelezwa na shirika la
EMEDO katika mikoa ya Mwanza, Mara na Kagera katika kipindi cha miaka
mitatu hadi mwaka 2025 kwa ufadhili wa taasisi ya RLNI- Life Boats ya
nchini Uingereza.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG

Post a Comment