Mradi wa kuzuia watu kuzama maji Ziwa Victoria watambulishwa Mwanza


Shirika la mazingira na maendeleo EMEDO limeutambulisha mradi wa kuzuia watu kuzama maji katika Ziwa Victoria kwa wadau mbalimbali wa uvuvi mkoani Mwanza.

Afisa Mradi huo, Arthur Mgema amesema lengo ni kuzuia vifo vitokanavyo watu kuzama maji katika Ziwa Victoria hasa wavuvi, watoto na wanawake wachakataji wa mazao ya samaki/ dagaa ambao wako kwenye hatari zaidi.

Akifungua kikao cha kuutambulisha mradi huo, Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Elikana Balandya amesema matukio ya watu kuzama maji yanazuilika endapo kila mmoja atatimiza wajibu wake.

Amesema kwa Mkoa Mwanza Serikali inatekelezeka mpango wa BBT (Building Better Tomorrow) katika sekta ya ufugaji na uvuvi hivyo mradi wa kuzuia kuzama maji katika Ziwa Victoria utasaidia kutoa elimu ili kuzuia vifo zitokanavyo na kuzama maji.

Mradi wa kuzuia kuzama maji katika Ziwa Victoria unatekelezwa na shirika la EMEDO katika mikoa ya Mwanza, Mara na Kagera katika kipindi cha miaka mitatu hadi mwaka 2025 kwa ufadhili wa taasisi ya RLNI- Life Boats ya nchini Uingereza.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG

No comments