Profesa Jay apokewa bungeni kwa shangwe
Jay, ambaye aliishi katika Chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) katika Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam kwa changamoto ya Figo kwa zaidi ya siku 400, alifika bungeni kwa ajili ya kuitambulisha Taasisi yake ya Profesa Jay Foundation, ambayo itajihusisha na uchangishaji wa fedha kwa ajili ya kusaidia matibabu ya Figo.
Aidha, wabunge wakiongozwa na Spika, walikubaliana kumchangia mwanamuziki huyo ambaye pia aliwaalika wabunge kuhudhuria uzinduzi wa taasisi yake hiyo Novemba 24 mwaka huu, itakayofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Post a Comment