Marekani yathibitisha Hamas inaendesha harakati za kijeshi katika chumba cha chini cha Hospitali ya Al-Shifa

 

Marekani imesema ina habari kwamba Hamas ilikuwa ikiendesha kituo cha amri na udhibiti wa kijeshi katika chumba cha chini cha hospitali ya Al-Shifa katika mji wa Gaza.

John Kirby, mratibu wa kimkakati wa mawasiliano wa Baraza la Usalama la Kitaifa la Marekani, amesema Hamas huhifadhi silaha katika vyumba vya chini vya hospitali na hujitayarisha kwa shambulio la Israeli.

Hii ni mara ya kwanza kwa mshirika wake, Marekani, kuunga mkono kwa uhuru madai ya Israel kwamba Hamas ina kambi ya kijeshi iliyofichwa katika hospitali hiyo. Hamas inakanusha madai haya.

Tangazo hilo linakuja huku Israel ikikabiliwa na shinikizo kutoka kwa jumuiya ya kimataifa kuwalinda raia waliokwama hospitalini.

Hapo awali, Rais wa Marekani Joe Biden alisema Hospitali ya Al Shifa "lazima ilindwe" kutokana na mapigano makali yanayoizunguka, huku Waziri Mkuu wa Uingereza Rishi Sunak akisema Israel lazima ichukue hatua kwa mujibu wa sheria za kimataifa.

Eneo linalozunguka Hospitali ya Al Shifa, kubwa zaidi huko Gaza, limekuwa kitovu cha mapigano katika siku za hivi karibuni. Maelfu ya watu wanaaminika kuwa wamejihifadhi katika hospitali ya Al Shifa.

No comments