Clemence Mtenga:Familia ya Mtanzania aliyefariki Gaza yazungumza
Familia ya Marehemu Clemence Mtenga inasubiri Serikali ifanye taratibu za usafirishaji wa mwili wa marehemu kutoka nchini Israel ili waweze kufanya maziko.
Clemence alikuwa miongoni mwa wanafunzi wawili kutoka Tanzania ambao Serikali ya Israeli hapo awali ilithibitisha kuwa walitekwa na kundi la Hamas baada ya shambulio la Oktoba 7.
Akizungumza na BBC, Msemaji wa familia ya marehemu, Boniface Mtenga alisema kuwa kwa sasa hakuna wanachoweza kukifanya mpaka pale serikali itakapowaambia lini mwili utakapofika nchini kwa ajili ya maziko.
Mtenga alisema, “Tulipata taarifa ya kifo cha kijana wetu siku ya Ijumaa, ambapo Mkuu wa Wilaya ya Rombo alifika nyumbani akiwa na ujumbe huo kutoka kwa serikali…
“…Tulipokea taarifa hiyo kwa majonzi kwasababu tumeondokewa na kijana wetu ambaye ndio kwanza alianza kupambania ndoto zake za maisha. Kwa sasa hatuna cha kufanya mpaka pale serikali itakapotuletea mwili kwa ajili ya maziko,” alisema Mtenga na kuongeza kuwa wanatarajia kuwa leo watapata taarifa rasmi ya lini mwili utakapowasili.

Post a Comment