wallace Karia wa Hispania afungiwa miaka mitatu na fifa. Busu la mrembo lamponza

 

Rais wa zamani wa shirikisho la soka nchini Uhispania Luis Rubiales amepigwa marufuku na Fifa kujihusisha na soka kwa miaka mitatu.

Rubiales alimbusu mshambuliaji Jenni Hermoso kwenye midomo kufuatia ushindi wa fainali ya Kombe la Dunia la Wanawake wa Uhispania dhidi ya England.

Busu hilo, ambalo mshambuliaji Hermoso anasema halikuwa la maafikiano, lilizua kelele, na hatimaye Rubiales alijiondoa kwenye jukumu lake mnamo Septemba.

Hermoso baadaye aliwasilisha malalamiko ya kisheria dhidi ya Rubiales.

Siku ya Jumatatu, shirikisho la soka duniani Fifa lilitangaza marufuku ya miaka mitatu kwa kukiuka kifungu cha 13 cha kanuni zake za nidhamu.

Rubiales anasema ananuia kukata rufaa dhidi ya marufuku hiyo.

“Nitakwenda hatua ya mwisho kuona haki inatendeka na ukweli unadhihirika,” alisema kwenye mitandao ya kijamii.

Fifa ilithibitisha kesi dhidi yake ilihusu "matukio yaliyotokea wakati wa fainali ya Kombe la Dunia la Wanawake la Fifa mnamo tarehe 20 Agosti 2023, ambapo Bw Rubiales alikuwa amesimamishwa kwa muda wa siku 90".

"Fifa inasisitiza dhamira yake kamili ya kuheshimu na kulinda uadilifu wa watu wote na kuhakikisha kuwa kanuni za msingi za maadili zinafuatwa," ilisema taarifa hiyo.


No comments