Lori 100 za misaada zinahitajika kwa siku huko Gaza - UN
Mashirika ya misaada yanasema Gaza inahitaji msaada zaidi kuliko malori 20 ya awali yaliyotangazwa na Rais Biden wa Marekani alipokuwa akisafiri kwa ndege kutoka Israel.
Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya kibinadamu, Martin Griffiths, anasema takriban lori 100 kwa siku zitahitajika.
Misri imekubali kufungua tena kivuko chake cha mpaka na Gaza ili kuruhusu usafirishaji kupita, ingawa maandalizi ya hili yanachukua muda.
Mawasiliano ya kidiplomasia kuhusu msaada kwa Wapalestina yanaendelea, ambapo rais wa Misri Abdul Fattah al-Sisi anatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mfalme Abdullah wa Jordan leo.
Misri na Jordan zimekuwa na amani na Israeli kwa miaka mingi na zimecheza majukumu muhimu ya upatanishi katika migogoro ya hapo awali.


Post a Comment