UGANDA KUTUNGA SHERIA MPYA KUDHIBITI USHOGA

Kenia | LGBTQ | ugandische Flüchtlinge in Kakuma

Uganda itapendekeza mswada mpya wa sheria kupinga vitendo vya mapenzi ya jinsia moja, huku mitandao ya kijamii ikijaa uvumi kwamba kuna makundi ya kimataifa ya kukuza ushoga yapo nchini humo.

Spika wa bunge Annet Anita Among hapo jana alichapisha kwenye mtandao wa Twitter video ya mkutano wa maombi alioshiriki, akisema Uganda italinda maadili na utamaduni wake kwa njia zote. Serikali za Magharibi na mashirika ya misaada yanayohudumu Uganda mara kwa mara hutuhumiwa kwa kuhimiza ushoga katika taifa hilo la Afrika Mashariki, na yamekuwa yakiitetea jamii ya watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja dhidi ya mashambulizi yanayohusishwa na mtindo wao wa kimahusiano.
DW
 

 

No comments