BINTI ATOZWA FAINI YA MILIONI NANE KUMFUATA RONALDO UWANJANI

SHIRIKISHO la mpira wa miguu
nchini Ireland FAI limempiga faini ya Irish £2500 (Milioni 8.3) shabiki mtoto
Addison Whelan (11) kwa kitendo chake cha kuvamia eneo la kuchezea (Pitch)
wakati timu yao ilipovaana na Ureno katika mchezo wa kuwania tiketi ya
kushiriki Kombe la dunia 2022 nchini Qatar.
Kupitia kituo cha Redio cha
FM104 Addison Whelan amesema "Nimepigwa faini kwa kosa la kuingia
uwanjani, baba anaenda kulipa"
"Niliingia uwanjani na
kumkimbilia Ronaldo, walinzi walikuwa wananifuata nyumba na wengine wakitokea
pembeni yangu"
"Nikawa naita jina la
Ronaldo, kwa bahati nzuri akanisikia na kunigeukia, akawaambia walinzi
waniache"
"Nilipofika nikamwambia,
mimi ni shabiki wako mkubwa, naomba jezi yako, akanipa"
Hivyo ndivyo ndoto ya mtoto wa
kike ilivyotimia

Post a Comment