WIZARA YA UJENZI NA JWTZ ZAAHIDI KUKUZA USHIRIKIANO
Waziri wa Ujenzi na
Uchukuzi, Mhandisi Dkt. Leonard Chamuriho, ameliombaJeshi la Wananchi Tanzania
(JWTZ), kuendelea kutoa ushirikiano kwa Wizara yake katika
utekelezaji wa miradi
mbalimbali inayosimamiwa na
Wizara hiyo nchini.
Akizungumza katika
kikao cha kufahamiana
na kubadilishana uzoefu
na Mnadhimu Mkuu wa
Jeshi la Wananchi
Tanzania (JWTZ), Luteni
Jenerali Methew Edward Mkingile, Dkt.
Chamuriho, amesema kuwa licha ya Wizara kutumia wataalam mbalimbali katika
miradi ya Ujenzi, bado inahitaji ushirikiano na
wataalam kutoka katika Jeshi hilo.
“Nakupongeza kwa
uteuzi uliopata, naamini kuwa uteuzi huu utakuwa chachu ya kuendeleza ushirikiano
tuliokuwa nao na
kusaidia katika mwendelezo
wa utekelezaji wa miradi
inayosimamiwa na Wizara”,
amesema Waziri Dkt.Chamuriho.
Aidha, Dkt.
Chamuriho amesisitiza kuwa
kutumia wataalam shirikishi
kutoka katika Jeshi hilo
imekuwa ni msaada
mkubwa katika kuhakikisha
miradi inatekelezwa kwa kuzingatia thamani ya fedha na kukamilika kwa
wakati. Kwa upande wake, Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Luteni
Jenerali Methew Edward Mkingile, ameipongeza Wizara hiyo kwa kutoaushirikiano
wa kutosha kwa Jeshi hilo na kuwaamini katika kutekeleza miradi yaWizara.
“Sisi tupo tayari
na bado tutaendelea kutoa ushirikiano kwa Wizara na Taasisi za Serikali kama
Sheria inavyotutaka, lengo ni kuhakikisha malengo na maendeleo ya nchi
yanafikiwa”, amesisitiza Luteni Jenerali Mkingile.
Uongozi wa
Wizara umekutana na
Mnadhimu Mkuu wa
Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali
Methew Edward Mkingile, ikiwa ni siku kadhaa mara baada ya uteuzi wake ambapo
pamoja na mambo mengine ziara hii ilikuwa na lengo la kuendeleza na kukuza
ushirikiano baina ya Taasisi hizo.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano
Serikalini, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi.

Post a Comment