WAZIRI MKUU KUHOJIWA KWA MAUAJI YA RAIS

MWENDESHA Mashtaka Mkuu Nchini Haiti amemtaka Waziri
Mkuu, Ariel Henry kueleza sababu za kuzungumza kwa simu na mmoja wa washukiwa
wa mauaji ya Rais Jovenel Moise usiku wa tukio (Julai 7)
Barua iliyoandikwa kwa maneno ya hadhari inasema Henry
alizungumza mara kadhaa kwa simu na mshukiwa mkuu, Joseph Felix Badio ambaye
bado anatafutwa, alipokuwa karibu na eneo la mauaji.
Barua hiyo iliyotumwa Septemba 10, 2021 inasema "ingawa
ni rais pekee ndiye mwenye mamlaka ya kuamuru kuitwa kwenye mahojiano kwa mtu
mwenye cheo chako, lakini kwa sasa Haiti haina Rais, nami nakualika kuhudhuria
na kutoa ushirikiano."

Post a Comment