SAFARI ZA NDEGE ZAREJEA TENA AFGHANISTAN

 International and domestic commercial flights resume in Afghanistan - CGTN

SAFARI za ndege za kimataifa zimeanza tena nchini Afghanistan ikiwa hatua muhimu kwenye juhudi za Serikali mpya ya Taliban kurejesha hali ya kawaida baada ya kuchukua madaraka mwezi uliopita.

Ndege ya Shirika la Qatar iliondoka jana kuelekea Doha ikiwa na abiria 113 wakiwemo Raia wa Ujerumani, Marekani, Canada na Uingereza na nyingine ya pili imetua Kabul leo.

Msemaji wa Wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani Ned Price amethibitisha kuwa Raia 10 na Wakaazi 11 wa kudumu wa Nchi hiyo walikuwemo kwenye ndege hiyo, Mjumbe maalum wa Qatar nchini Afghanistan, Mutlaq bin Majed al-Qahtani, amesema safari hii ni ya kawaida na si sehemu ya kampeni ya kuwahamisha watu wanaotaka kuikimbia Afghanistan.

Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Qatar, Sheikh Mohammed bin Abdulrahman Al-Thani amewashukuru Viongozi wa Taliban kwa kusaidia kwenye kuufungua tena uwanja mkubwa wa ndege wa Kabul. 
#MillardAyoUPDATES


No comments