RAIS AMTEUA DK. STERGOMENA KUWA MBUNGE

 Rais Samia akutana na Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Katibu Mtendaji wa  SADC) | JamiiForums

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Dkt. Stergomena Lawrence Tax kuwa Mbunge wa Bunge la .Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Septemba 10, 2021.

Mhe. Dkt. Tax ameteuliwa kutoka kwenye nafasi kumi za Wabunge wa Kuteuliwa na Rais.

Kabla ya uteuzi huo, Mhe. Dkt. Tax alikuwa Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) ambaye amemaliza muda wake mwezi Agosti, 2021.


No comments