KOREA KASKAZINI YAFANYA GWARIDE LA MIAKA 73 BILA KUONYESHA SILAHA

TOFAUTI na ilivyo kawaida, Korea
Kaskazini imefanya maonesho ya gwaride la kuadhimisha miaka 73 tangu kuasisiwa
kwa taifa hilo, lakini haikuonyesha silaha.
Kinyume na ilivyo kawaida jeshi la taifa
halikuonesha makombora yake ya masafa marefu mara hii. Aidha hakukuwa na mbwa wa ulinzi au wale wa kuwinda
wala vifaru vya kijeshi.
Badala yake wanajeshi walivalia magwanda ya
kujikinga dhidi ya maambukizi ya maradhi yanayosambaa kwa hewa kama yale
yanayotumika katika wadi za wagonjwa wa Covid19 ila zote zilikuwa za rangi ya
chungwa.
Rais Kim Jong-un alihudhuria sherehe hizo, lakini
hakuzungumza kama kawaida yake huku akionekana kuwa amepoteza uzani.
Wachambuzi wa siasa wanasema serikali ya Korea
Kaskazini inataka kuonesha dunia kwamba juhudi zake kwa sasa zimeelekezwa zaidi
katika masuala ya ndani ya nchi.

Post a Comment