POLEPOLE AHOJIWA NA KAMATI YA MAADILI CCM, AKATAA KUSEMA KILICHOJIRI KIKAONI

 HUMPHREY Polepole Ateuliwa Kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM | UDAKU  SPECIAL

MBUNGE wa kuteuliwa na Rais, Humprey Polepole leo alifika mbele ya Kamati ya Maadili ya Wabunge wa CCM, akiitika wito pamoja na wenzake Jerry Silaa na Josephat Gwajima ambao Bunge lilipitisha azimio la kuwasimamisha kwa mikutano miwili kutokana na tuhuma za kusema uongo na kushusha hadhi na heshima ya Bunge, mahojiano yanafanyika leo Dodoma.

Baada ya kumaliza mahojiano hayo, mbunge huyo ambaye aliwahi kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, alitoka na kukutana na waandishi wa habari ambao walipomuuliza nini kimejiri, alijibu.. "Utaratibu wa chama chetu kikao cha maadili ni kikao cha ndani, kwa hiyo taarifa zote zitatoka kwa utaratibu wa Chama”

No comments