NUGAZ APUNGIWA MKONO YANGA, ALIYESABABISHA AAJIRIWE KUSHIKA MIKOBA YAKE

 Mpira sio Chumvi, mashabiki tulieni - Antonio Nugaz (+Video) - Bongo5.com

 

ANTONIO Nugaz, Afisa Mhamasishaji wa klabu ya Yanga, ambaye aliajiriwa ili apambane na aliyekuwa mhamasishaji wa Simba wakati huo, amemaliza mkataba wake na waajiri hao hawana nia ya kumuongeza muda.

Taarifa zilizopatikana mida hii zinasema Nugaz amepewa shukurani na uongozi huo kwa kazi kubwa na iliyotukuka, lakini wamemalizana naye na nafasi yake sasa inachukuliwa na Haji Manara ambaye atakiongoza kitengo cha uhamasishaji.

No comments