MBOWE, WENZAKE WATATU WAWASILI MAHAKAMA KUU KWA KESI YAO LEO

MWENYEKITI wa Chama Cha Demokrasia
na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake watatu, wamewasili Mahakama
Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi leo kuendelea kusikiliza
kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili.
Mbowe na wenzake wanatakiwa kuwa mahakamani hapo leo baada ya
kesi yao kusimama kwa siku nne kutokana na Jaji Elinaza Luvanda kujitoa
kuisikiliza. Jaji huyo alijitoa Jumatatu baada ya washtakiwa kutokuwa na imani
naye kwamba hawaamini kama atawatendea haki baada ya kutupilia mbali
mapingamizi waliyoweka.
Mahakama sasa imemteua Jaji Mustapha Siyani kusikiliza kesi
hiyo. Kwa mujibu wa hati ya wito, kesi itaendelea leo mahakamani hapo.

Post a Comment