BEKI WA ZAMANI BAYERN ANUSURIKA JELA MIAKA MITANO, ALIMWA FAINI BILIONI 4

JEROME Boateng,
beki wa zamani wa Klabu za Man City, Bayern Munich na Ujerumani, amenusurika
kifungo cha miaka mitano jela, lakini amelazimika kulipa faini ya paundi
milioni 1.5, sawa na bilioni nne na ushee kwa fedha za Tanzania kwa kosa la
kumpiga na kumsababishia maumivu mzazi mwenzake.
Boateng, 33, anadaiwa kumfanyia vitendo
hivyo mchumba wake wa zamani, Sherin Senler wakiwa katika visiwa vya Caribbean
mapumzikoni miaka mitatu iliyopita.
Senler, mama wa watoto wawili mapacha,
aliiambia mahakama kwamba alipigwa usoni hadi damu kutoka na kubanwa kifuani
kiasi cha kushindwa kupumua.
Boetang alikataa tuhuma zote na kudai
kuwa ni yeye ndiye aliyekuwa akinyanyasika katika uhusiano wao.
731

Post a Comment