MASHAHIDI WANNE WA UTETEZI KESI YA MBOWE KUFICHWA

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania
Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu "Mahakama ya Mafisadi"
imekubaliana na maombi ya upande wa utetezi wa kuficha Mashahidi wao wanne
katika kesi ya uhujumu uchumi na ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA
Freeman Mbowe na wenzake.
Jaji Mustapha Siyani ameahirisha
kesi hiyo hadi Septemba 15, 2021 ambapo itasikilizwa mfululizo ambapo upande wa
utetezi una mashahidi 7 huku wanne wakiwa wamefichwa.

Post a Comment