MAHUDHURIO YA WALIMU SASA KUHAKIKIWA KIELEKTRONIKI NCHI NZIMA

WAZIRI wa Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Ummy Mwalimu amesema Serikali inakusudia kuandaa
mfumo wa kielektoniki wa alama za vidole kwa ajili ya kuhakiki mahudhurio ya
Walimu kwenye shule mbalimbali za Tanzania.
Ummy amesema mpango huo ni kwa Shule zote za Msingi na
Sekondari katika Halmashauri zote nchini ili kudhibiti mahudhurio ya Walimu
Mashuleni, ametoa kauli hii wakati akifungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi
Tawi la Tume ya Utumishi wa Walimu Dodoma.

Post a Comment