JUMA UBAO AFARIKI DUNIA

 Inaweza kuwa picha ya Mtu 1, anacheza ala ya muziki na gitaa

MWANAMUZIKI mkongwe wa muziki wa dansi ambaye pia ni mwenyekiti wa chama cha muziki wa Dansi (CHAMUDATA) Juma Ubao amefariki dunia leo asubuhi.

Juma Ubao aliyejulikana pia kama King Makusa, enzi za uhai wake alitamba zaidi na bendi Biashara Jazz "Dunda Dunda".

Aidha, Juma Ubao ambaye alikuwa mwimbaji na mcharaza gitaa mahiri, alitamba pia na kundi la 'zing zong' lililojulikana kama The Six Manyara kwa kushirikiana na Hassan Rehan Bitchuka.

Taarifa za msiba wa Juma Ubao zimetolewa na Katibu wa CHAMUDATA Hassan Msumari.

Said Mdoe 11/9/2021

 

No comments