JANUARY MAKAMBA, MAKAME MBARAWA WAREJEA BARAZA LA MAWAZIRI

RAIS Samia Suluhu amefanya mabadiliko madogo kwenye baraza
la Mawaziri na mwanasheria mkuu wa Serikali kama ifuatavyo.
1.
Rais Samia Suluhu amemteua Dkt. Stergomena Tax kuwa Waziri wa
Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, anachukua nafasi ya marehemu Elias Kwandikwa
2.
Dkt. Ashatu Kijaji ameteuliwa kuwa waziri wa Habari, Mawasiliano
na Teknolojia ya habari kuchukua nafasi ya Dkt. Faustine Ndugulile ambae uteuzi
wake umetenguliwa
3.
January Makamba anachukua nafasi ya Merdard Kalemani wizara ya
Nishati
4.
Makame Mbarawa anachukua nafasi ya Chamuriho wizara ya ujenzi na
uchukuzi
5.
Dkt. Feleshi anachukua nafasi ya Kilangi kuwa Mwanasheria mkuu
wa Serikali

Post a Comment