JOE BIDEN, XI JINPING WAONGEA BAADA YA MIEZI SABA

 US Biden and China's Xi hold first call in seven months - BBC News

 

RAIS wa Marekani Joe Biden alizungumza na Rais Xi Jinping wa China jana jioni kwa mara ya kwanza ndani ya kipindi cha miezi saba, wakijaribu kuuepusha ushindani uliopo baina yao kugeuka kuwa mgogoro.

Viongozi hao wawili walikuwa na majadiliano mapana na ya kimkakati ambapo walijadili maeneo ambayo masilahi yao hukutana, na maeneo ambayo masilahi yao, maadili na mitazamo yao hutofautiana.

Ikulu ya Marekani, White House, ilisema kwenye mazungumzo hayo kwa njia ya simu, ujumbe wa Biden ulikuwa ni kwamba Marekani inataka kuhakikisha ushindani baina ya mataifa hayo makubwa duniani unasalia kwenye kiwango ambacho hakutakuwa na hali yoyote ya kuwaingiza kwenye mgogoro usiokusudiwa.

Mazungumzo hayo ni ya kwanza baina ya viongozi hao tangu mwezi Februari, walipozungumza kwa masaa mawili muda mfupi baada ya rais Joe Biden kumrithi Donald Trump

No comments