MLIPUKO MWINGINE WATOKEA KABUL

Ripoti kutoka Kabul Afghanistan
leo jioni zinasema umetokea mlipuko nje ya uwanja wa ndege wa Kabul ambako
maelfu ya watu wamekusanyika kujaribu kuikimbia nchi hiyo kwa kutumia ndege za
mataifa ya Magharibi tangu Taliban wachukue nchi mwezi huu.
Msemaji wa Wizara ya ulinzi ya
Marekani Pentagon John Kirby amethibitisha taarifa za mlipuko huo lakini
madhara ya mlipuko huo bado hayajafahamika ila limetajwa kuwa ni shambulio la
kujitoa muhanga.
Mataifa ya magharibi yalikuwa
tayari yameonya juu ya uwezekano wa shambulio katika uwanja wa ndege wa Kabul
saa kadhaa zilizopita wakihusisha shambulio hilo na kundi la Afghanistan lenye
mafungamano na kundi linalojiita Dola la Kiislamu IS ambalo uwezekano wa
kufanya shambulio hilo umetokana na Taliban kuwaachia huru Wafungwa wengi ambao
miongoni mwao wamo wa wa kundi hilo.

Post a Comment