MAGORI AIZUNGUMZIA SIMBA, MO

 Inaweza kuwa picha ya Mtu 1 na maandishi yanayosema 'EXCLUSIVE INTERVIEW Crescentius Magori'

 

MJUMBE wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Crescentius Magori akiongea na Simba App jana, amezungumzia masuala kadha ya klabu ya Simba sc juu ya Kambi, Usajili pamoja na maendeleo kiujumla.

 

1.Kuhusu Kambi.

Magori amesema kuwa klabu ya Simba sc imefanikiwa kuweka kambi ya siku 14 yenye mafanikio makubwa , kwani kambi ilikuwa na kila kitu kuanzia Gym mpaka viwanja vya mazoezi vye hadhi kubwa, kwa Mujibu wa Magori amesema kuwa timu ilifikia kwenye hoteli ya Nyota 5 na walikuwa wanafanya mazoezi kwenye viwanja bora kabisa ambavyo ni vya Mohamed wa VI ambavyo timu yoyote Duniani inaweza kuvitumia.

Ameendele kusema kuwa kwa mujibu wa Ratiba Simba sc imehitimisha kambi hii leo na muda wowote wataondoka kurejea Tanzania kwa ajili ya kambi nyingine kwa ajili ya kuzoea Mazingira ya Afrika Mashariki kwa wachezaji wao wapya.Pia amesema kuwa Wanafurahi kucheza michezo miwili migumu kwa sababu FA Rabaat na Olympiques ni timu za daraja la Juu Nchini Morocco.

Kuhusu USAJILI.

Magori amesema kuwa Simba sc imesajili Vijana wenye njaa kubwa , wanaviwango Vikubwa sana, Magori amewasifia wachezaji Wote waliosajiliwa akieleza sifa zao .Amesema kuwa Sakho ana attibutes zote za King Kibadeni ni winga wa kisasa mwenye kasi nguvu na akili kubwa njee ya 18 , amemsifia pia Heneck Inonga beki toka DC Motemapembe beki ambaye anacheza miguu yote miwili huku akiwa na utulivu mkubwa sana.Amemuelezea Peter Banda kuwa ni hatari sana hasa kutokana na Spidi yake , feints , Agility na uwezo mkubwa wa kufanya maamuzi sahihi ndani ya 18 huku akimuelezea Dancani Nyoni Kama mchezaji anayekuja kuleta radha tofauti kutokana na uwezo wake wa kupiga kwa kushitukiza eneo lolote huku akitumia mguu wa kushoto kama silaha.

Kuhusu Maendeleo

Magori amesema kuwa , Jana wamezindua Simba APP kama sehemu ya mpango mkakati wa klabu kidigitali , amesema mpaka jana Tsh 15M zilikuwa tayali zimekusanywa kupitia APP tu huku akiwaomba wanasimba kupakuwa APP hiyo kwa ajili ya Exclusive interviews.

Ameendelea kusema kuwa anashanga watu kumsema Vibaya Mo Dewji kuhusu kuposti vitu vya Simba sc , amesema kuwa kikatiba Mo Dewji ni kiongozi wa Simba sc hivyo anahaki yakufanya hivyo halafu Mo ni mshabiki wa Simba sc tangu akiwa mdogo so haiwezi kuwa ajabu.

 

No comments