GOLIKIPA PETER SHILTON AELEZEA ALIVYOATHIRIKA KWA KAMARI
]

MLINDA mlango nyota
wa zamani wa England, ambaye ndiye mchezaji aliyecheza mechi nyingi zaidi za
timu ya taifa hilo, Peter Shilton, amezungumzia tabia yake ya kucheza kamari
ambayo imemfanya kupoteza mamilioni ya shilingi.
Katika mahojiano
maalum na gazeti la Daily Mail, mwanasoka huyo ambaye alimshukuru mwanamke mpya
aliyempata ambaye aliweza kumponya maradhi hayo, amesema anafikiri amepoteza
kiasi cha kama paundi za Uingereza laki nane (sawa na shilingi za kitanzania
bilioni 2.4) katika kipindi chote alichocheza kamari yaani betting.
"Betting ni
ugonjwa mbaya, ukianza kuumwa huwezi kuacha. Ni addiction kama addictions
zingine," anasema Shilton, ambaye alikuwepo langoni wakati marehemu Diego
Maradona akifunga bao maarufu la Mkono wa Mungu nchini Mexico mwaka 1986 wakati
wa fainali za kombe la dunia.

Post a Comment