WAZIRI ASHAMBULIWA, BINTIYE, DEREVA WAFA

HALI ya usalama inaonekana kuendelea kuwa tete nchini Uganda baada ya msafara wa Waziri wa Ujenzi, Jenerali Katumba Wamala kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana karibu na nyumbani kwake Mjini Kampala.
Mtoto wake, Brenda Wamala Nantongo na Dereva, Haruna Kayondo,
wameripotiwa kupoteza maisha kufuatia tukio hilo. Mashuhuda wamesema
walioshambulia walikuwa kwenye pikipiki.
Jenerali Wamala alikuwa Mkuu wa Jeshi la UPDF mwaka 2013 hadi
2017 baadaye akapewa Cheo cha Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi.

Post a Comment