MTANDAO WA WANAOIBA MAFUTA WABAINIKA


Watu watano wakamatwa sakata la Bomba la Mafuta. – swahili afrika 24


WABONGO BWANA! Ukaguzi uliofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni umebaini nyumba moja iliyopo Ulongozi ina vifaa vya kuchimba visima, lakini vinatumika kuchimba kuelekea Bomba la Mafuta.

Katika Ukaguzi huo vifaa mbalimbali vimegundulika yakiwemo magari yanayosadikiwa kutumika kubeba mafuta kutoka eneo wanalochimbia na kuyasambaza maeneo mbalimbali jijini Dar.

Nyumba inayotumika kufanya shughuli hizo imekutwa na ulinzi mkubwa wa Kamera na walinzi japo hapakuwa na shughuli yoyote inayoendelea ndani. Imeelezwa, aliyepanga nyumba analipa Tsh. Milioni 60 kwa mwaka kama Kodi.

No comments