TUNDU LISSU: ROMA MKATOLIKI NA NEY NI BORA KULIKO DIAMOND

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu ameibuka na kusema hawezi kumuunga mkono Diamond Platinums kwa vile licha ya ukubwa wa kazi yake, lakini hajawahi kusimama kwenye haki au kupinga maovu ya nchi hii.
Kupitia katika ukurasa wake wa mitandao
ya kijamii aliandika.. "Mapenzi hayalazimishwi na uzalendo sio kuunga
mkono kila kitu cha nchi yako hata kama hakistahili. Diamond platinumzi sio
Roma mkatoliki au Neytrueboy au mrithi wa Bob Marley. Hajawahi kusimama kwenye
haki au kupinga maovu ya nchi hii. Mimi binafsi simuungi mkono."

Post a Comment