TUNDU LISSU ATAKA SABAYA ATENDEWE HAKI


Tanzania's Tundu Lissu: Surviving an assassination attempt to run for  president - BBC News

MWANASHERIA maarufu nchini, ambaye pia alikuwa mgombea wa Urais wa uchaguzi uliopita kupitia upinzani, Tundu Lissu, ametaka haki kutendeka katika kushughulikia suala la aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Ole Sabaya.

Sabaya anashikiliwa na vyombo vya dola akihojiwa kwa tuhuma kadhaa zinazomkabili, akiwa mikononi kwa zaidi ya wiki moja iliyopita.

Katika akaunti yake kwenye mtandao wa Twitter, Lisu anayeishi uhamishoni Ubelgiji, alisema pamoja na mabaya yote yanayosemwa juu ya Sabaya, kitendo cha kushikiliwa bila kufikishwa mahakamani ni ukiukwaji wa haki za binadamu.

"Kumuweka ndani kwa wiki nzima ni kukiuka sheria zetu na kuendeleza tabia ya ukiukwaji wa haki za binadamu wa vyombo vyetu vya usalama."

No comments