ALIYESIMAMISHWA AREJESHWA YANGA


Wakili Simon Patrick 1⃣ Anatajwa kuzungumza na moja ya viongozi Simba bila  idhini ya uongozi kutoka Yanga. 2⃣ Inaelezwa sakata… – SPORTS NEWS

WAKILI Simon Patrick, ambaye alisimamishwa na Klabu yake ya Yanga katika nafasi ya Ukurugenzi wa Sheria na Wanachama amerejeshwa kufuatia Kamati Huru iliyoundwa kuchunguza tuhuma dhidi yake, kutobaini lolote.

Taarifa iliyotolewa na klabu hiyo usiku wa jana, imesema Kamati huru iliyoongozwa na Wakili Raymond Wawa, haikubaini lolote katika tuhuma zilizoelekezwa kwa Simon na hivyo baada ya kujadiliana kwa kina, Kamati ya Utendaji imejiridhisha pasi na shaka kwamba Wakili Simon Patrick hakuwa na hatia katika tuhuma zilizopelekea kusimamishwa kazi Novemba 18 mwaka jana.

No comments