STELLA MANYANYA AMTETEA ALIYEFUKUZWA BUNGENI

BAADA ya Mbunge Condester kufukuzwa bungeni jana kwa madai ya kuvaa nguo zisizo na staha bungeni, mbunge wa Nyasa, Injinia Stella Manyanya ameamua kusimama na kumtetea;
"Jambo lililonifanya nizungumze
mimi Mtu mzima leo ni kilichotokea leo asubuhi ilibidi nifuatilie kwa karibu
sana kwenye mitandao, hivi hiyo nguo ilikuaje? hali halisi ikoje? baadae
niliishia kusononeka, Vijana kama hawa sisi wenyewe tumesema waingie Bungeni
lakini hatutegemei kijana aingie Bungeni amevaa gauni tulilokuwa tunalivaa sisi
zamani”
“Vijana lazima wachukuliwe kwa ujana wao ili mradi hizo nguo
wanazovaa ziwe na heshima yake, hata jana wakati tunapitisha bajeti ya Wizara
ya Habari, Sanaa, Utakaduni na Michezo limezungumzwa jambo tena wakaenda mbali
wakasema acheni Vijana wapige kiki zao lakini hii haikuwa kiki lilikuwa ni vazi
nadhifu la kijana”
“Sitegemei wote sisi tutavaa vitenge, sitegemei wote sisi
tutaamka tutavaa dera kila Mtu na utamaduni wake ili mradi liwe vazi la
heshima, labda pengine niseme kwamba kuomba radhi ni sawa lakini mimi
ningeshauri kwa sababu ya mazingira ya kiutu uzima pengine na yeye aliyetoa
hoja kwa sababu ya uzoefu wake alitegemea atuone wote tuko vile pengine sio
lazima sana tukamuamsha atuombe radhi lakini la msingi tuone jambo
lililotendeka leo sio la haki"

Post a Comment