NATAKA SPIDI MRADI MWENDOKASI- RAIS SAMIA


MNACHELEWESHA UCHUMI"-RAIS SAMIA USO KWA USO NA MKANDARASI WA MRADI WA  MWENDOKASI MBAGALA - YouTube

RAIS Samia Suluhu Hassa amemtaka mkandarasi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka kuelekea Mbagala kuongeza kasi ya ujenzi wake, kwani amesisitiza ya sasa hairidhishi.

Akiwa katika eneo la Mbagala Zakhem ambako alifanya ukaguzi wa mradi huo alisema;
“Nilikuwa napitia mafaili ya miradi ofisini nikauona mradi huu wa mwendokasi Mbagala, mradi huu kwa sasa ulikuwa ufikie asilimia karibu 60 na kitu lakini kwa taarifa nilizopata leo mradi upo kwenye asilimia 16 tu, nikasema tuje tuone kinachokwamisha mradi huu.

“Tumeongea na Wasimamizi wa mradi huu wa mwendokasi Mbagala na pia Wakandarasi na tumeona kinachokwamisha mradi, Serikali bado hatujaridhishwa na kasi yake ingawa mwishomwisho hapa wameongeza speed kidogo, tumekubaliana waongeze kasi zaidi ili mradi umalizike

“Tunataka mradi huu wa mwendokasi Mbagala umalizike ili kurahisisha safari zenu Wananchi na tuinue uchumi, Serikali juzijuzi hapa tumembadilisha Kiongozi mkubwa wa mradi huu tumemuweka mwingine ili atusaidie kuongeza kasi ya mradi huu”

 

 

No comments