SABAYA HAYUPO PEKE YAKE, NAO WAKAMATWE

TAASISI ya Kupambana na Kudhibiti Rushwa ikiwa inaendelea na mahojiano na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya, wananchi toka pembe zote wametaka mamlaka kuwakamata na viongozi wengine ambao wanaamini walikuwa na tabia kama za mteule huyo wa Hayati John Magufuli.
Katika mitandao
mbalimbali ya kijamii, wananchi hao wanadai tuhuma za rushwa, vitisho kwa
wafanyabiashara, utekaji nyara, kutesa na maovu mengine anayotuhumiwa nayo
Sabaya, yamefanywa na wateule wengi wa serikali ya awamu ya tano na kutaka nao
wakamatwe.
Majina kadhaa
yamekuwa yakitajwa yakiwahusisha viongozi hao, wakiwemo mawazili, wakuu wa
mikoa na wilaya aingawa hata hivyo, jina la mkuu mmoja wa mkoa na mwingine wa
wilaya, yamekuwa yakijirudia zaidi wakitakiwa kuchukuliwa na vyombo vya dola
ili kuhojiwa na kufikishwa mahakamani.

Post a Comment