SABAYA ASOMEWA MASHTAKA SITA, APELEKWA MAHABUSU WIKI MBILI

 

2797548_Tutamtoa_Mkoloni_Mweusi_Soon_freedom_fighter_2025_posted_on_Instagram__Jun_4_2021_at_1...jpg

ALIYEKUWA Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, amesomewa mashtaka sita akiwa pamoja na wenzake watano yakiwemo makosa yasiyo na dhamana na hivyo atakaa mahabusu kwa muda wa wiki mbili hadi Juni 18, mwaka huu kesi yake itakapotajwa tena.

Miongoni mwa mashtaka aliyosomewa ni pamoja na uhalifu wa kutumia silaha, utakatishaji fedha, uhujumu uchumi, rushwa na kuongoza genge la uhalifu.

Mashtaka hayo alisomewa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Arusha.

 

No comments