RAIS SAMIA SULUHU HASSAN APOKEA UJUMBE WA PAUL KAGAME WA RWANDA

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo Juni 3 mwaka
huu, amepokea salamu maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Paul Kagame.
Katika ujumbe huo uliowasilishwa na Mjumbe maalumu Vincent Biruta, Rais Kagame
alitoa pole kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt John Magufuli , alimpongeza kwa kupokea kijiti cha Urais na pia
alimuhakikishia kuwa Rwanda itaimarisha ushirikiano na Tanzania.

Post a Comment