MECHI YA SIMBA VS YANGA JULAI 3 IPO HAIPO
MECHI ya mzunguko wa pili kati ya watani wa jadi wa soka nchini, Simba na Yanga, iliyopangwa kupigwa Julai 3 mwaka huu, haina uhakika wa kuwepo kutokana na viongozi wa Jangwani kuanza kuleta hofu.
Msemaji wa Yanga,
Hassan Bumbuli amesikika akiiambia redio moja ya mtandaoni kuwa wao wamebakiza
mechi nne ili kumaliza Ligi Kuu na kati ya hizo, ile ya Simba hawaitambui.
Kauli hiyo imezua
taharuki kiasi cha kupelekea Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Almas Kasongo kutoa
tahadhari kwa Yanga kuzingatia kanuni, lakini shaka zaidi imekuja baada ya
Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, kwanza kuibuka na kuikana kauli ya Bumbuli, lakini
akatia mashaka zaidi aliposema;
"Uongozi wa
Yanga utatoa taarifa rasmi juu ya msimamo wake kuelekea mechi hiyo."
MECHI IPO AU HAIPO?

Post a Comment