JOKATE FULL MAUJIKO WILAYANI KISARAWE


Shule.jpg

MKUU wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo ambaye wakati akiteuliwa kushika nafasi hiyo alipokewa kwa hisia tofauti, hivi sasa anapewa sifa kama mmoja wa viongozi vijana wenye uwezo mkubwa wa kufanya kazi za maendeleo.

Katika kipindi chake cha uongozi, mrembo huyo namba mbili wa Miss Tanzania mwaka 2006, ameipaisha wilaya hiyo katika nyanja za elimu na uchumi.


Kisarawe ni moja kati ya halmashauri tisa za mkoa wa Pwani ikiwa imeanzishwa tarehe 1 Julai 1907. Wilaya ya Kisarawe inapakana na Wilaya ya Mkuranga kwa upande wa Kusini-mashariki na Wilaya ya Morogoro upande wa Magharibi. Mashariki-Kaskazini kuna Jiji la Dar es Salaam, Kaskazini Wilaya ya Kibaha na Kusini Wilaya ya Rufiji. Lakini Utafikiri Kisarawe ndo Mkoa kumbe ni Wilaya tu kati ya Wilaya 9.

Pamoja na kukuta watu wa Pwani ni wavivu, kwa muda mchache aliokaa Kisarawe, ameitambulisha kimataifa. Kisarawe imekuwa Maarufu.

Baadhi ya mambo ambayo ameyafanya na yanaonekana.

Elimu

Wanafunzi walikuwa watoro na Shule za Kisarawe zilikuwa zinafanya vibaya, lakini sasa zinafanya vizuri.

Wilaya ya Kisarawe aliikuta ina uhitaji wa madawati 1166 ambapo kwa sekondari uhitaji ni 484, na 642
kwa shule ya msingi. Kafanyia kazi

Alikuta wilaya ina uhitaji wa shilingi milioni 124 kwa ajili ya kujenga matundu ya vyoo 113 Mashuleni, kafanyia kazi

Alikuta Wilaya inauhitaji wa ofisi za walimu za kisasa katika shule 14 ambazo zinagharimu shilingi milioni 880. Kafanyia kazi

Alikuta Wilaya haina Maktaba, zinajengwa.

 Alikuta Kisarawe ina matatizo ya Maji. Kwa muda mfupi tatizo la Maji limepungua.

Huduma za afya zimeboreka hasa huduma ya Mama na Mtoto. Ujenzi wa Wodi ya Upasuaji.

Huduma ya Umeme imeboreka nk.

Ameweza kufanya mambo ya Maendeleo bila kuwasumbua vyama pinzani wala kujenga chuki kwa wananchi. Hajihusishi na Ufusadi. Ana heshima kwa Kila mtu na ni msikivu.

Jokate ni Mfano kwa Viongozi wanaoteuliwa sasa.


No comments