MARUFUKU KUUZA DAWA KWENYE MABASI
SERIKALI imepiga marufuku tabia sugu
ya baadhi ya watu kuuza dawa zinazotibu magonjwa mbalimbali kwenye vyombo vya
usafiri, hasa mabasi ya mikoani na kuonya kuwa atakayebainika kuuza au kununua,
atatozwa faini ya hadi milioni kumi.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Dawa na
Vifaa Tiba, Adam Fimbo, amesema ni marufuku abiria kununua dawa mbalimbali hasa
za kutibu magonjwa zinazouzwa kwenye magari na vyombo vingine vya usafiri na
kwamba endapo mnunuzi na muuzaji watakamatwa watachukuliwa sheria.
Mkurugenzi huyo amesema kabla ya kutumia dawa inapaswa mtu
kupata ushauri wa wataalamu wa afya ikiwa ni pamoja na kupata vipimo.
"Kwanza hilo haliruhusiwi kutangaza dawa kwenye vyombo
vya usafiri, lazima upate ushauri wa daktari upime kwanza, natoa wito tena
hairuhusiwi kuuza wala kununua,” alisisitiza Adam Fimbo

Post a Comment