MANJI MIKONONI MWA TAKUKURU
SIKU moja tu baada ya kurejea nchini akitokea ughaibuni alikokwenda kwa muda wa miaka kadhaa, mfanyabiashara maarufu nchini, Yussuf Mehboob Manji, amefikia mikononi mwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU.
Kwa mujibu wa
gazeti la Mwananchi toleo la leo Juni 3, 2021, inadaiwa tuhuma zinazomkabili ni
tatu, zikiwemo ukwepaji kodi na fedha za Klabu ya Yanga ambayo alikuwa
Mwenyekiti wake na mfadhili wake mkubwa.
Mkurugenzi wa
taasisi hiyo, Kamanda Hamduni alikiri kuwa walimkamata juzi uwanja wa ndege
mara tu baada ya kutua na kwamba hawajui lini watamuachia, kwani hiyo itatokana
na jinsi mahojiano yakatavyokuwa.

Post a Comment