JUMA NYOSO ANAPITWA NA WAKATI

BAADA ya kupewa kadi ya pili ya njano na baadaye nyekundu kwa kumchezea faulo beki wa Simba, mashabiki wengi nchini wanasema nahodha wa Ruvu Shooting, Juma Nyoso anapitwa na wakati akiwa bado kijana.
Nyoso alimfuata na
kumpiga kitu kama kofi beki Shomari Kapombe, wakati akienda kuufuata mpira
uliotoka nje. Ingawa haikuonekana kama ni kitu kikubwa kwa Kapombe, beki huyo
alilala chini kuonyesha kuumia na mwamuzi akampa Nyoso kadi ya njano, ikiwa ni
ya pili katika mchezo huo kabla ya kumpa nyekundu itakayomfanya kukaa nje mechi
mbili kati ya nne ambazo timu yake imebakiza.
"Nyoso
mshamba, anacheza mpira wa kizamani katika mazingira ya kisasa. Wachezaji kama
hao watajiondoa wenyewe," anasema shabiki wa soka John David akiiambia
Ojuku Blog.
"Michezo kama
hiyo wanachezaga watu wenye vipaji, siyo mtu butua butua kama Nyoso, mimi
ningekuwa kiongozi wa Ruvu Shooting hiyo ndiyo ingekuwa mechi yake ya
mwisho," anasema shabiki mwingine, Nasri Inno.

Post a Comment