HIZI NDIZO SABABU HASA ZA MANJI KUKAMATWA


Quality Group Tycoon Manji Owns 99% of Tigo Tanzania - Lawyers -  allAfrica.com

 HUKU kukiwa na maswali mengi mtaani juu ya nini hasa kinaendelea kati ya mfanyabiashara mkubwa nchini, Yussuf Mehboob Manji na dola, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), ambayo ndiyo inamshikilia, imetoa taarifa zifuatazo.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Takukuru Kamishna wa Polisi Said Hamduni, Manji anashikiliwa toka alipowasili nchini Tanzania akituhumiwa kwa makosa yafuatayo; 

1) Kukwepa kodi :


Kampuni zake za Intertrade Commercial LTD Service na Golden Globe International Service Limited zinatuhumiwa kwa kutolipa kodi ya VAT kati ya mwaka 2011 na 2015. 

2) Udanganyifu wakati wa manunuzi ya hisa za kampuni ya Tigo.

3) Kupitia kampuni yake ya Quality Group kuna maswali kuhusu mapato ya klabu ya Yanga ambayo alikuwa akiidhamini na kuiongoza kama mwenyekiti wakati huo.

4) Kuhujumu usalama wa taifa kwa kukutwa na vitambaa vinavyotengeza sare za jeshi la wananchi wa Tanzania JWTZ vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 200 za Kitanzania.

Manji aliondoka nje ya nchi mwaka wa 2018 baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam kumuachia huru pamoja na wenzie watatu Septemba 2017 walipokuwa wakituhumiwa kwa makosa saba ya uhujumu uchumi.


No comments