GSM WAMKARIBISHA YUSSUF MANJI YANGA

MKURUGENZI wa Uwekezaji wa Kampuni
ya GSM, Injiinia Hersi Said amesema wanamkaribisha kwa mikono miwili na moyo
mweupe kabisa, mfanyabiashara maarufu Yussuf Manji kurejea Yanga.
Akihojiwa na kituo cha redio cha Efm
cha Sports HQ, Hersi alisema kwa sasa kampuni hiyo inagharamikia kila kitu kwa
sasa ndani ya klabu hiyo, ikiwa ni pamoja na mishahara kwa asilimia mia moja,
kambi, usafiri, usajili na kadhalika.
"Akitokea mtu akaja akasema
nyinyi GSM fanya hivi, mimi nitagharamia huku, tunamkaribisha kwa mikono
miwili, lengo letu kubwa na la msingi ni kuhakikisha klabu hii inasonga
mbele," alisema.

Post a Comment