ALIYEMUUA MMAREKANI MWEUSI JELA MIAKA 30

WAENDESHA Mashtaka wa Jimbo la Minnesota wanaomba mshukiwa wa mauaji ya George Floyd, Derek Chauvin apewe adhabu ya miaka 30 gerezani.
Hivyo, kwa mujibu wa Tmz kuna uwezekano mkubwa mtuhumiwa huyo
kutumikia kifungo cha robo ya karne gerezani, ikiwa waendesha mashtaka hao
watafikia uamuzi huo.
Katika tukio lililotokea Mei 2020, Chauvin alinaswa kwenye
ukanda wa video akiwa amepiga goti juu ya shingo ya Bwana Floyd, Mmarekani
mweusi, katika mji wa Minneapolis hadi kupelekea kifo, na kuchochea maandamano
Marekani na dunia kote kupinga ukatili unaotekelezwa na polisi pamoja na
ubaguzi wa rangi.

Post a Comment