34 WADAKWA WIZI WA KUKWAPUA SIMU, MIKOBA KWA BODABODA MORO


Vijana 3 mbaroni mauaji dereva wa bodaboda

VIJANA wapatao 34 wamekamatwa na Jeshi la Polisi mkoa wa Morogoro kwa tuhuma za wizi wa kukwapua mali za wananchi kwa kutumia pikipiki ambapo jumla ya pikipiki nane zinashikiliwa na jeshi hilo.

Kwa mujibu wa Fortunatus Musilimu ambaye ni RPC Morogoro, vijana hao wamedakwa katika maeneo ya Mji Mpya, Mwembesonga, Kidabaga na Mtawala.

Inadaiwa vijana hao hupakizana wawili kwenye pikipiki hizo na kuvizia watembea kwa miguu wanaoongea na simu au walioshika mikoba na kuikwapua.

Katika hatua nyingine SACP Musilimu, amesema jeshi hilo linawashikilia watu watatu kwa tuhuma ya wizi wa vifaa vya ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR ikiwemo vipande vya nyaya za shaba mpya na zilizounguzwa huku nyingine zikiwa zimefumuliwa kwenye 'transfomer' zenye jumla ya uzito wa kilogramu77.9 zilizokuwa zimehifadhiwa katika ghala la mfanyabiashara aliyefahamika kwa jina moja la Ahmed lililopo mtaa wa Modeco Manispaa ya Morogoro.

No comments