SIMBA OUT CHAMPIONS LEAGUE

TIMU ya soka ya Simba, ikicheza soka safi na la kuvutia imeifunga Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini kwa bao 3-0 katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, ushindi ambao hata hivyo, imeitoa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika msimu huu.
Katika mchezo wa
awali uliofanyika Johannesburg, mabingwa hao wa Tanzania walipigwa bao 4-0 na
hivyo Kaizer Chiefs wanaingia nusu fainali ya michuano hiyo mikubwa kabisa kwa
ngazi ya klabu barani Afrika.
Mabao ya Simba
yalifungwa na nahodha John Bocco aliyetupia mawili na moja kutoka kwa Clatus
Chota Chama.

Post a Comment